Wednesday 28 September 2016

BALOZI WA MALAWI TANZANIA HAWA NDILOWE ATEMBELEA MKOA WA SONGWE

Balozi wa Malawi nchini Tanzania Hawa Ndilowe akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa  katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa zilizopo Vwawa, Mbozi, Songwe tarehe 28 Septemba, 2016.


Balozi Hawa Ndilowe akiandika katika kitabu cha Wageni Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa Chiku Gallawa.


Mkuu wa Mkoa Chiku Gallawa akitoa taarifa ya Mkoa wa Songwe kwa  Balozi Hawa Ndilowe


Balozi Hawa Ndilowe akitoa maelezo ya lengo la ziara yake katika Mkoa wa Songwe. 

 Maelezo ya Balozi Hawa Ndilowe yalijikita katika kuboresha ushirikiano kati ya wananchi  wenye kipato cha chini  ambao wamekuwa wakiishi kwa amani na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili za Malawi na Tanzania kwa muda mrefu.  Ziara ya Balozi huyo ilibeba vipaumbele katika nyanja za Kilimo, Utalii, Ushirikiano kati ya Wilaya na Wilaya, Mkoa na Mkoa vilevile Maswala ya Ulinzi na Usalama.  Aidha, muda mwingi ulitumika kujadili maswala ya Kilimo na Mifugo ambapo baadhi ya maazimio yaliyojitokeza ilikuwa kufikiria namna ya kubadilishana uzoefu wenye mafanikio bora ili kumkwamua mkulima wa kipato cha chini katika upatikanaji wa pembejeo, Uzalishaji na upatikanaji wa Soko sahihi.


Baada ya Maongezi, Walitakiana Kheri katika kudumisha Urafiki, Upendo, Mafanikio ya mwanzo wa safari ya ushirikiano uliowekwa msingi na Balozi wa Malawi Tanzania na Hawa Ndilowe na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa (aliyevaa miwani katika mstari wa mbele) akiwa na Balozi wa Malawi Tanzania Hawa Ndilowe  (kushoto kwake) katika picha ya pamoja na  Makatibu, Wataalam na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Songwe

No comments:

Post a Comment