Monday 19 September 2016

BARAZA KAMILI LA MADIWANI SONGWE

kikao cha kwanza cha Baraza kamili la Waheshimiwa Madiwani wa wilaya ya Songwe kilifanyika tarehe 15 Septemba, 2016 katika ukumbi wa Chuo cha Uuguzi Mwambani  uliopo Mkwajuni Songwe.


Viongozi iliyosheheni viongozi mbalimbali 



Kushoto: Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Godfrey Kawacha na Elias Nawera Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Songwe.




Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samwel Jeremiah


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe Elias Nawera



Wazee wakaribishwa; wa kwanza kulia, Ismail Isack Nguwingwa mwenyekiti wa mila Tarafa ya Kwimba


Hatimaye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe  apatikana.

Na Mwandishi wetu.

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Songwe lilimchagua  Diwani Abraham Kugaluka kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Halmashauri hiyo. Baada  ya kutoa neno la  shukrani Mwenyekiti Kagaluka aliitaka TAMISEMI kuwapa motisha watumishi walioshika nafasi za kukaimu ukuu wa Idara wenye sifa zinazostahili wathibitishwe ili waendelee na Idara zao kwa ufanisi zaidi.

Vilevile aliongeza kuwa Serikali ishughulikie stahili za malipo kwa Watumishi kwani kwa kufanya hivyo itapelekea Watumishi kuwa na moyo wa kufanya kazi kwa bidii  hasa katika kipindi hiki cha kuanzisha Wilaya ya Songwe.

 Mwenyekiti Kugaluka alimalizia kwa kuwataka Waheshimiwa Madiwani, Watumishi wa Serikali na Wananchi wote wa Songwe kuvunja makundi ya Siasa na kuanza kufanya kazi kwa manufaa ya wananchi " Hapa kazi tu" alisisitiza.


No comments:

Post a Comment