Monday 31 October 2016

MWANAFUNZI MLEMAVU WA VIUNGO AKABIDHIWA BAISKELI YA KUSUKUMA SEKONDARI YA NALYELYE MBOZI






Afisa Elimu Elimu Maalum Erick Mbunda akitoa akieleza umuhimu wa kusaidia wanafunzi wenye ulemavu kwa sababu wana uwezo sawa na  wanafunzi wengine. Afisa Elimu alitoa maelezo hayo kwa njia ya kutamka kwa maneno na lugha ya alama



Afisa Elimu, Elimu Maalumu Erick Mbunda akimkabidhi Joshua Haonga Baiskeli ya kusukuma

Joshua Haonga akishukuru baada ya kupewa baiskeli ya kusukuma


Mkuu wa shule ya Sekondari ya Nalyelye Rozi Alberto Mwakyoma akitoa rai kwa wadau mbalimbali alisema "  Kama itawezekana Joshua angehamishiwa kwenye shule ya Bweni kwani mazingira ya shule hii na nyumbani kwa mlezi wake hairidhishi" aliomba


Mwalimu Elizabeth Mwankemwa alisema " Joshua anajitahidi sana katika taaluma na anashirikiana vizuri na wanafunzi "

 Dada mkuu wa shule Esther Mtega alikiri kuwa wanashirikiana vizuri na wenzake pia wanafuzi wote wanampenda Joshua kiasi ambacho wanamchangia anapokuwa amepungukiwa vifaa vya shule kama daftari, Kalamu n.k vilevile wanamsukuma kwenye baiskeli bila kulazimishwa.


Noel Kasebele vilevile alikiri kama Dada Mkuu ila alitoa ombi kwa Serikali na Wadau mbalimbali kuongeza misaada zaidi kwa Joshua

MLEMAVU WA VIUNGO JOSHUA SAMSON HAONGA APATIWA BAISKELI

Na mwandishi wetu.

Joshua ni mwanafunzi ambaye ni  yatima na mlemavu wa viungo, anasoma katika kidatu cha pili katika shule ya Sekondari ya Nalyelye iliyo katika kata ya Mlowo, wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe
Erick Mbunda Afisa  Elimu Elimu Maalum alitoa msaada wa kiti baiskeli ya kusukumwa baada ya kuona matatizo aliyokuwa akiyapata mwanafunzi huyo kupitia kwa Waalimu.
Aidha Mbunda alisema kuwa aliomba msaada wa baiskeli hiyo kutoka kwa msamalia mwema anayeishi Njombe ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Afisa huyo alisema kuwa amekuwa akisaidia wanafunzi wenye ulemamvu na wasio wanafunzi bila kujali umri wao. Vilevile aliwashukuru wanafunzi na Waalimu kwa moyo wao wa kumsaidia Joshua wakati akitumia baiskeli iliyokuwa inaharibika mara kwa mara.

Mwalimu Mkuu Roze Alberto Mwakyoma alisema, pamoja na misaada inayotolewa kutoka kwa Waalimu, Wanafunzi na Mdau huyo, alitoa  rai kuwa Joshua angeweza kufanya vizuri kama angepata shule ya wenye uhitaji kama Yeye au Shule ya Bweni kwa  sababu mvua zikinyesha anashindwa kufika shuleni pia mazingira ya nyumbani kwa mlezi wake hayawezi kufanana na bweni.

Mlezi wa Joshua alikiri kuwa hana uwezo wa kumlea Joshua inavyotakiwa, alisema “ mimi nina watoto wengi na maisha yangu na mke wangu ni biashara ndogo na kilimo wakata Joshua anakiwa kuwa na mtu jirani kwani hawezi kujihudumia kwa lolote, pia choo change  sababu ana watoto wengi na maisha yao yanategemea kilimo na biashara ndogo wakati huo Joshua hawezi kujitegemea kwa lolote hata kwenda chooni hawezi kwenda mwenyewe. Naomba serikali inisaidie inisaidie” alisisitiza.




Bustani ya Shule ya Nalyelye yenye miche 2400 katika kutekeleza agizo la Mkoa la kuotesha miche ya miti 2000 kwa kila Shule


Tuesday 25 October 2016

KATIBU TAWALA WA MKOA WA SONGWE AKABIDHIWA MADAWATI 400 NA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU NYANDA ZA JUU KUSINI

Sherehe ya kukabidhi Madawati kutoka kwa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) zilizofanyika kwenye viwanja vya Ofisi za Mkuu wa Mkoa Songwe   tarehe 25 Oktoba, 2016.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Kanda Nyanda za juu Kusini Denis Kweslema akitoa taarifa  kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Eliya M. Ntandu kuhusu mchango wa Madawati.

Katibu Tawala wa Mkoa akikata utepe kama ishara ya kuzindua sherehe ya kukabidhiwa madawati


Katibu Tawala wa Mkoa akipeana mikono na Kamu Meneja wa TFS baada ya kukabidhiwa madawati 400

Katibu Tawala akitoa neno la shukrani kwa mchango aliokabidhiwa kutoka kwa Wakala wa Huduma za Misitu na Wadau mbalimbali. katika shukrani zake alisema " Madawati haya tutayasambaza kwa kuzingatia mahitaji" aliongeza kwa kutoa wito kwa wadau wengine kutoa michango kwa sababu bado kuna mahitaji ya madawati, Mabati na Saruji katika huduma za Elimu na Afya Mkoani Songwe.

Picha ya pamoja ya Katibu Tawala, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa, Wakurugenzi wa Wilaya na Timu ya Huduma za Misitu Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Picha ya pamoja ya Katibu Tawala, Timu ya Huduma za Misitu, Wataalam Ofisi ya Sekretarieti ya Mkoa na Wakurugenzi wa Wilaya za Mkoa wa Songwe.

KIKAO KAZI CHA KAMATI ZA MITIHINANI ZA HALMASHAURI ZA WILAYA MKOA WA SONGWE

Kikao cha kazi  cha Kamati Za Mitihani  Mkoa wa Songwe kuhusu Maandalizi, Mapokezi, Ugawaji na Usimamizi wa mitihani  ya kidato cha nne kilichofanyika tarehe 25 Oktoba, 2016 kwenye Ukumbi wa  Halmashauri ya  Wilaya ya Mbozi,  Songwe. 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Eliya M. Ntandu akitoa maelekezo kwa wanasemina. Katibu Tawala aliwasisitiza washiriki wa kikao umuhimu wa Uadilifu, Uaminifu, Ushirikiano katika zoezi zima la Mitihani.







Washiriki wakisikiliza kwa umakini


Sunday 23 October 2016

CHIFU WA KABILA LA WABUNGU KATIKA UTATUZI WA MIGOGORO MKWAJUNI

Chifu wa Kabila la Wabungu Chifu Mwamvongo (aliyeshika finbo, kavaa kofia ya kijani na njano) akiwa na Wazee wa Mila kabla ya kuanza kikao cha kutatua mgogoro wa mahali pa kuzika Machifu.

Chifu Mwavongo akitoa ufafanuzi kuhusu uhalali wa eneo la kufanyia mazishi la Amaponga kuwa lipo katika Kata ya Mwambani na  eneo hilo limekuwa likitumika tangu miaka 130 iliyopita. Kikao hicho kiliamua kuwa eneo hilo litatumika kwa ajili ya kuzikia Machifu tu. kikao hicho kilimkaribisha Afisa utamaduni , Michezo na Vijana wa Wilaya ya Songwe Sia Kisamo ( mwenye gauni lenye rangi ya njano na weusi) tarehe 21 Oktoba, 2016.


SIKU YA USAFI MKWAJUNI, SONGWE



Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samwel Jeremiah (Aliyevaa shati la Kitenge na Kofia nyeupe) akiongoza Wataalam na  wananchi katika zoezi la usafi wa Mazingira Mkwajuni, Songwe tarehe 22 Oktoba, 2016



Tuesday 11 October 2016

ZIARA YA MKUU WA MKOA CHIKU GALLAWA KATIKA KATA YA KAPELE








Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa  akifanya mkutano katika a Kijiji cha Chipumpu.  tarehe 05/10/2016

Mkuu wa Mkoa akifafanua umuhimu wa kuacha kilimo cha mazoea na kuanza kilimo biashara.


 Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa alifanya ziara katika vijiji vya Chipumpu, Kapele na Kasinde ambavyo vipo katika kata ya kapele Wilaya ya Momba Mkoa wa Songwe tarehe 05 Oktoba, 2016. Mkuu wa mkoa aliongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Songwe na wataalam wa Sekretarieti ya Mkoa na Wataalamu wa Wilaya ya Momba.
Katika ziara hii Mkuu wa Mkoa alihamasisha suala la maendeleo katika vijiji hivyo na kueleza dhamira ya Serikali kutoka katika kipato cha chini kwenda katika kipato cha kati. Vilevile kuipeleka Tanzania katika nchi ya Viwanda ifikapo 2025.
 Aidha, Chiku Gallawa alitumia muda huo kujiridhisha kwa Wananchi kama mihtasari iliyo wasilishwa na Mwekezaji Nkusu Theo Sugar Limited ilikuwa ni ridhaa ya pande zote mbili kati ya Mwekezaji na Wananchi.

Mkutano katika kijiji cha Kapele

Mkuu wa Mkoa akitoa ufafanuzi kwa wananchi umuhimu wa kutunza mazingira. kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Songwe Juma Irandu na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mwaijulu J.D

Mkuu wa Mkoa alikemea ukataji wa miti kiholela unaoendelea katika kijiji. Hivyo kukemea wahamiaji wakifugaji wanaohamia bila kufata taratibu na viongozi wanao wakaribisha bila kufuata utaratibu. Alisisitiza kuwa kila mhamiaji atakayetaka kuhamia hapo kijijini ajadiliwe kwenye  mkutano Mkuu wa Kijiji  na wanayo mamlaka ya kumkubali na kumkataa.

Mkutano katika kijiji cha Kasinde


 Mkuu wa Mkoa akisisitiza kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kukifanya Kijiji cha Kasinde kuwa kijiji cha Biashara.


Mkuu wa Mkoa aliwaeleza wananchi kwamba, Serikali imedhamiria kuhama kutoka uchumi wa chini mpaka uchumi wa kati kwa kuhakikisha kipato cha mtu mmoja mmoja kinakua. Watu wawe na kipato kuanzia milioni 6 mpaka milioni 20. Alisema “ sasa tunaanza na urasimishaji wa ardhi ili kila mwananchi awe na hati ya eneo lake. Hivyo hatutakiwi kuanza kuuza ardhi yetu kwa sasa. Kwa kuwa kwa ekari moja mnavuna gunia 15 za mpunga, inabidi mvune gunia 45 kwa ekari moja. Yatupasa kukifanya kijiji cha Kasinde kiwe kijiji biashara”.  Mkuu wa Mkoa aliwakumbusha wananchi kuwa Mkoa umeanza kukusanya takwimu  kwa ajili ya kupanga maendeleo ya kimkoa. Pia aliongeza kuwa kijiji kianze kusimamia katika kutunza mazingira. Aliagiza kuwa  “tuache kukata miti ovyo, Pia tuache kukaribisha wageni bila kufuata utaratibu ili kuzuia migogoro isiyo ya lazima”. alisisitiza