Friday 7 October 2016

MKUU WA MKOA WA SONGWE CHIKU GALLAWA AKABIDHIWA MABATI NA KAMPUNI YA PRNG MINERAL LIMITED

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa akikabidhiwa mabati  1,200  kutoka kwa  Maneja wa Kampuni  ya  PRNG Mineral Limited Patrick Ochieng  tarehe 05 Oktoba, 2016 nje ya ofisi ya Mkuu  wa Mkoa iliyopo Vwawa, Mbozi.

Kampuni ya PRNG ipo katika mchakato wa kupata leseni ili ianze kuchimba rasmi madini ya sumaku yenye uwiano wa kipekee wa madini ya neodymium na praeseodymium.

Vilevile  katika eneo la kaskazini ya Ngualla kuna madini aina ya niobium - tantalium na phosphate. 

Mkuu wa Mkoa akitoa shukrani kwa Kampuni ya PRNG Mineral Limited.

 Katika shukrani hizo Mkuu wa Mkoa alisema misaada inayotolewa na wadau hupokelewa  katika mfumo wa serikali na kusambazwa kwenye miradi ambayo wananchi wametoa michango yao ya ujenzi wa maboma hadi kufikia hatua ya  kuezeka. Aidha alisema mpaka kipindi hiki Mkoa una upungufu wa mabati yasiyopungua 150, 000. Hatimaye alitoa wito kwa wadau mbalimbali kupenda kutoa michango ya aina mbalimbali  ili kuifikia Tanzania yenye uchumi wa kati na Viwanda mwaka 2025


Mkuu wa Mkoa Chiiku Gallawa akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa


Picha ya pamoja ya Mkuu wa Mkoa, Wawakilishi wa Kampuni ya PRNG Minerals Limited na Wataalam wa Sekretarieti ya Mkoa


No comments:

Post a Comment