Sunday 23 October 2016

CHIFU WA KABILA LA WABUNGU KATIKA UTATUZI WA MIGOGORO MKWAJUNI

Chifu wa Kabila la Wabungu Chifu Mwamvongo (aliyeshika finbo, kavaa kofia ya kijani na njano) akiwa na Wazee wa Mila kabla ya kuanza kikao cha kutatua mgogoro wa mahali pa kuzika Machifu.

Chifu Mwavongo akitoa ufafanuzi kuhusu uhalali wa eneo la kufanyia mazishi la Amaponga kuwa lipo katika Kata ya Mwambani na  eneo hilo limekuwa likitumika tangu miaka 130 iliyopita. Kikao hicho kiliamua kuwa eneo hilo litatumika kwa ajili ya kuzikia Machifu tu. kikao hicho kilimkaribisha Afisa utamaduni , Michezo na Vijana wa Wilaya ya Songwe Sia Kisamo ( mwenye gauni lenye rangi ya njano na weusi) tarehe 21 Oktoba, 2016.


No comments:

Post a Comment