Tuesday 11 October 2016

ZIARA YA MKUU WA MKOA CHIKU GALLAWA KATIKA KATA YA KAPELE








Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa  akifanya mkutano katika a Kijiji cha Chipumpu.  tarehe 05/10/2016

Mkuu wa Mkoa akifafanua umuhimu wa kuacha kilimo cha mazoea na kuanza kilimo biashara.


 Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa alifanya ziara katika vijiji vya Chipumpu, Kapele na Kasinde ambavyo vipo katika kata ya kapele Wilaya ya Momba Mkoa wa Songwe tarehe 05 Oktoba, 2016. Mkuu wa mkoa aliongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Songwe na wataalam wa Sekretarieti ya Mkoa na Wataalamu wa Wilaya ya Momba.
Katika ziara hii Mkuu wa Mkoa alihamasisha suala la maendeleo katika vijiji hivyo na kueleza dhamira ya Serikali kutoka katika kipato cha chini kwenda katika kipato cha kati. Vilevile kuipeleka Tanzania katika nchi ya Viwanda ifikapo 2025.
 Aidha, Chiku Gallawa alitumia muda huo kujiridhisha kwa Wananchi kama mihtasari iliyo wasilishwa na Mwekezaji Nkusu Theo Sugar Limited ilikuwa ni ridhaa ya pande zote mbili kati ya Mwekezaji na Wananchi.

Mkutano katika kijiji cha Kapele

Mkuu wa Mkoa akitoa ufafanuzi kwa wananchi umuhimu wa kutunza mazingira. kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Songwe Juma Irandu na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mwaijulu J.D

Mkuu wa Mkoa alikemea ukataji wa miti kiholela unaoendelea katika kijiji. Hivyo kukemea wahamiaji wakifugaji wanaohamia bila kufata taratibu na viongozi wanao wakaribisha bila kufuata utaratibu. Alisisitiza kuwa kila mhamiaji atakayetaka kuhamia hapo kijijini ajadiliwe kwenye  mkutano Mkuu wa Kijiji  na wanayo mamlaka ya kumkubali na kumkataa.

Mkutano katika kijiji cha Kasinde


 Mkuu wa Mkoa akisisitiza kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kukifanya Kijiji cha Kasinde kuwa kijiji cha Biashara.


Mkuu wa Mkoa aliwaeleza wananchi kwamba, Serikali imedhamiria kuhama kutoka uchumi wa chini mpaka uchumi wa kati kwa kuhakikisha kipato cha mtu mmoja mmoja kinakua. Watu wawe na kipato kuanzia milioni 6 mpaka milioni 20. Alisema “ sasa tunaanza na urasimishaji wa ardhi ili kila mwananchi awe na hati ya eneo lake. Hivyo hatutakiwi kuanza kuuza ardhi yetu kwa sasa. Kwa kuwa kwa ekari moja mnavuna gunia 15 za mpunga, inabidi mvune gunia 45 kwa ekari moja. Yatupasa kukifanya kijiji cha Kasinde kiwe kijiji biashara”.  Mkuu wa Mkoa aliwakumbusha wananchi kuwa Mkoa umeanza kukusanya takwimu  kwa ajili ya kupanga maendeleo ya kimkoa. Pia aliongeza kuwa kijiji kianze kusimamia katika kutunza mazingira. Aliagiza kuwa  “tuache kukata miti ovyo, Pia tuache kukaribisha wageni bila kufuata utaratibu ili kuzuia migogoro isiyo ya lazima”. alisisitiza

No comments:

Post a Comment