Tuesday 25 October 2016

KATIBU TAWALA WA MKOA WA SONGWE AKABIDHIWA MADAWATI 400 NA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU NYANDA ZA JUU KUSINI

Sherehe ya kukabidhi Madawati kutoka kwa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) zilizofanyika kwenye viwanja vya Ofisi za Mkuu wa Mkoa Songwe   tarehe 25 Oktoba, 2016.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Kanda Nyanda za juu Kusini Denis Kweslema akitoa taarifa  kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Eliya M. Ntandu kuhusu mchango wa Madawati.

Katibu Tawala wa Mkoa akikata utepe kama ishara ya kuzindua sherehe ya kukabidhiwa madawati


Katibu Tawala wa Mkoa akipeana mikono na Kamu Meneja wa TFS baada ya kukabidhiwa madawati 400

Katibu Tawala akitoa neno la shukrani kwa mchango aliokabidhiwa kutoka kwa Wakala wa Huduma za Misitu na Wadau mbalimbali. katika shukrani zake alisema " Madawati haya tutayasambaza kwa kuzingatia mahitaji" aliongeza kwa kutoa wito kwa wadau wengine kutoa michango kwa sababu bado kuna mahitaji ya madawati, Mabati na Saruji katika huduma za Elimu na Afya Mkoani Songwe.

Picha ya pamoja ya Katibu Tawala, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa, Wakurugenzi wa Wilaya na Timu ya Huduma za Misitu Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Picha ya pamoja ya Katibu Tawala, Timu ya Huduma za Misitu, Wataalam Ofisi ya Sekretarieti ya Mkoa na Wakurugenzi wa Wilaya za Mkoa wa Songwe.

No comments:

Post a Comment