Sunday 18 December 2016

ZIARA YA MKUU WA MKOA WILAYANI MBOZI TAREHE 16 DISEMBA, 2016

Mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa katika eneo la kuegesha Malori la Mamlaka ya Mji wa Vwawa, Mbozi, Songwe.


Chiku Gallawa akisikiliza Maswali kutoka kwa Wananchi

Mkuu wa Mkoa akijibu Maswali 

Mkuu wa Mkoa wa Sogwe Chiku Gallawa alifanya mkutano wa hadhara na Wananchi  ili kusikiliza kero zao na kuzitatua katika eneo la kituo cha kuegesha magari ya mizigo Vwawa, Mbozi
Katika kujibu kero za Wananchi alisema,
Kuhusu ardhi alisema, Mkakati wa Mkoa wa Songwe kwanza ni kukusanya takwimu na kutengeneza rasimu ya mkoa, pili  ni urasimishaji ardhi Mjini na Vijijini ili hata mkulima mdogo mwenye ekari mbili  awe na Hati yake. 
Mkurugenzi wa Wilaya ya Mbozi Mwaigomole alisema hati 33,000 zimetolewa kwa kushirikisha wananchi na Afisa Ardhi wa Mbozi  Simbeye aliongeza kuwa ramani ya mipango miji inaendelea kuandaliwa na Wananchi wataendelea kushirikishwa. 
Aidha mkuu wa Mkoa alisema mkoa wa Songwe umepanga kukamilisha urasimishaji ardhi katika miaka  mitatu hivyo aliwataka Halmashauri ya Mbozi kuazima Wataalam kutoka Halmashauri zingine ndani ya mkoa kusaidiana nao na siyo kungojea mradi ulete fedha ndiyo kazi ifanyike.
Kuhusu shida ya Maji katika Mamlaka ya Mji mdogo wa Mbozi Mkuu wa Mkoa alisema hilo tatizo linajulikana na ndiyo maana amemwalika Waziri mwenye dhamana ili asaidie kutatua tatizo hilo wakati huu  wananchi wajitahidi kuvuna na kutumia maji ya mvua kwenye mabati ya nyumba.
Vilevile alisema matatizo ya Mama Lishe kwanza yapitie kwa Mkuu wa Wilaya kabla ya kufika kwake. Na kuingiliana maeneo ya kibiashara yatatuliwe na Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi.
Chiku Gallawa akichambua utata wa eneo ambalo ofisi  ya Mkuu wa Mkoa itajengwa ambalo limepelekea gumzo kwa wakazi wa Mamlaka za miji ya Vwawa na Mlowo, alifafanua   kuwa, kuna tofauti ya tafsiri ya Makao makuu ya Mkoa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, alisema Makao Makuu ya Mkoa yamekubaliwa kuwa katika  eneo la Vwawa ambalo litalelewa na Manispaa ambayo itaunganisha Mamlaka za Miji ya Vwawa na Mlowo na kwamba Makao makuu yahusisha Taasisi mbalimbali na kati ya hizo ni  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Hospitali ya Mkoa, chuo cha VETA,  Magereza, Polisi, Uhamiaji, na zinginezo. Aliongeza kuwa mpaka sasa maeneo manne yametambuliwa na yanasubili wataalam wa Mipango Miji na Udongo wapime na kutoa mapendekezo ya mwonekano wa makao makuu na aina ya majengo kutona na aina ya udongo.
Baada ya hapo wapi ngazi husika zitashirikishwa kutoa maamuzi. 

No comments:

Post a Comment