Tuesday 20 December 2016

MKUU WA MKOA CHIKU GALLAWA AKUTANA NA WATUMISHI WA HALMASHARURI YA WILAYA YA MBOZI

Mkuu wa Mkoa Chiku Gallawa akiongea na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kwenye Ukumbi wa Halmashauri tarehe 17 Disemba, 2016.

Afisa Maendeleo wa Wilaya ya Mbozi Dakawa akitoa taarifa ya Idara yake





Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa akiwa katika ziara zake za kawaida kutembelea Halmashauri za wilaya za Songwe alitembelea wilaya ya Mbozi tarehe 16 Disemba, 2016 ambapo alikutana na Wakuu wa Idara kwa lengo la  kuwabadilisha kifikra ili waweze kupanga mikakati ya kuongeza kipato cha Wananchi tofauti na utaratibu uliozoeleka

Chiku Gallawa hakuridhishwa na taarifa zilizokuwa zinatolewa na Wakuu Idara  kwa sababu hazikuwa na takwimu sahihi. Vilevile  jinsi walivyozoea kufanya kazi, alisema “Wataalam msing’ang’anie kufanya  vitu ambavyo havitoi matokeo ambayo serikali inategemea wapate  wananchi”. Alisisitiza.

Alishauri Wataalam wafunguke kwa kusoma wengine wanafanya nini.
Aliagiza kila Idara iandae mkakati  ya Idara katika wiki moja na kuwakilisha kwake kupitia kwa mkuu wa Wilaya.

Vilevile aliagiza kuwa Watumishi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Kilimo, Mapato waende vijijini ili warudi ili waandae mikakati yao.wapangiwe kata ili kurahisisha shughuli za maendeleo kwa wanachi na kwamba shughuli za uratibu wa miradi zifanyike kutoka katika kata.
Upande wa Mazingira alisema Mtaalam anayeratibu kitengo hicho ameshindwa kusimamia ipasavyo hivyo  alimwagiza Mkurugenzi ampangie kazi nyingine.

Aidha aliongeza kuwa hati chafu katika Wilaya ya Mbozi inatokana na wafanyakazi wanaofanya kazi kwa mazoea.

Vilevile aliagiza kuwa NGO zote zitambuliwe katika Halmashauri na kujua shughuli zao pamoja na bajeti ili kutorudia kazi ambazo Halmashauri inatekeleza.


No comments:

Post a Comment