Friday 10 March 2017

MKUU WA WILAYA YA SONGWE ARIDHISHWA NA UFAULU WA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI YA MAWENI

 Mkuu wa Wilaya ya Songwe  Samwel Jeremiah akiongea na Wanafunzi wa  shule ya sekondari ya Maweni


Mkuu wa Wilaya akiwa katika picha ya pamoja Walimu na Wanafunzi 

Na Sia Kisamo: Afisa Utamaduni Songwe

Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samwel Jeremiah akiwapongeza wanafunzi wa Shule ya sekondari Maweni kidato cha sita kwa kufanya vizuri katika mashindano ya Mock Mkoa wa Songwe ambapo shule hiyo ilishika nafasi ya nne kimkoa kati ya shule 12 zilizoshiriki mashindano ya mitihani hiyo. Mkuu wa Wilaya aliwatia moyo  Waalimu na wanafunzi na kuwaambia Waalimu waongeze juhudi katika ufundishaji na  wanafunzi wajitahidi kusoma kwa bidii na kuzingatia masomo.
Pia Mkuu wa Wilaya hiyo alisema wanafunzi waliofanya vizuri na kushika nafasi ya kumi bora wanaandaliwa zawadi na kuwaahidi kuwa wanafunzi watakaofanya vizuri zaidi katika mtihani wa Taifa watapata nafasi mbili za kusoma USA na China.

No comments:

Post a Comment