Tuesday 28 February 2017

TAASISI YA KIFEDHA YA BAYPORT YATOA MSAADA WA KOMPYUTA KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGWE

Meneja wa  Taasisi ya fedha ya Bayport kanda za juu kusini  Emmanuel Nzutu (aliyevaa shati jeupe wa nne kutoka kulia ) akimkabidhi Kompyuta  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Songwe  Wakili Elias Nawera.


BAYPORT WATOA KOMPYUTA MBILI KWA AJILI YA MATUMIZI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGWE

Na Sia Kisamo -  Afisa Utamaduni Songwe

Katika makabidhiano hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe na kuhudhuriwa na baadhi ya Wataalam, Meneja wa Taasisi hiyo alisema kuwa, wanathamini utendaji wa Halmashauri kwa maendeleo ya wananchi ndiyo maana wameamua kutoa msaada wa Kompyuta mbili za mezani  ili  kurasisha utekeleza wake.
Naye Mkurugenzi wa Wilaya alitoa shukrani na kuwataka waendelee kutoa ushirikiano katika nyanja mbalimbali ili kutimiza adhma ya serikali kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2025.

No comments:

Post a Comment