Tuesday 7 February 2017

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGWE AZINDUA FILAMU YA KIKUNDI CHA FIGHTER ARTIST GROUP



Na Mwandishi wetu Sia  Kisamo - Songwe


Mkurugenzi wa Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe Elias Nawera akiinua DVD juu kama ishara ya kuzindua Filamu ya kikundi cha Fighters Artist Group cha Wilaya ya Songwe tarehe 05 Februari, 2017



Msanii wa Kikindi ... akisoma risala kwa Mkurugenzi wa Wilaya.

 Msanii .. alisema lengo la kuandaa filamu hiyo ni  kudumisha umoja na mshikamano kati ya wasanii na jamii, kutafuta soko la pamoja la sanaa, kulinda na kuendeleza utamaduni  na pia kushirikiana na taasisi mbalimbali zitakazokuwa tayari kusaidia uboreshaji wa sanaa kwa lengo la kujiongezea thamani na kuunganishwa na masoko yenye uhakika



Elias Nawera akipokea nakala ya risala baada ya kusomewa

 Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya akiongea na Wasanii baada ya uzinduzi



Mkurugenzi wa Wilaya akiwa katika picha ya pamoja na Wasanii wa Fighter Artist Group

Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa filamu inayoitwa "Tamati ya dunia

Katika hotuba hiyo Elias Nawera aliwahamasisha  wasanii kuhakikisha kuwa wanasajiliwa ili kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu za nchi, pia wawe na madhumuni mema ya kutumia sanaa kuelimisha jamii na  kujipatia kipato.

 Mwisho aliwasihi wasanii kuwa na kazi nyingine za uzalishaji mali mbali na sanaa kwa kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali ili kunufaika na mkopo  unaotolewa na halmashauri ya wilaya ya songwe kwa lengo kuwawezesha  vijana kujiongezea kipato.


No comments:

Post a Comment