Tuesday, 7 February 2017

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGWE AZINDUA FILAMU YA KIKUNDI CHA FIGHTER ARTIST GROUP



Na Mwandishi wetu Sia  Kisamo - Songwe


Mkurugenzi wa Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe Elias Nawera akiinua DVD juu kama ishara ya kuzindua Filamu ya kikundi cha Fighters Artist Group cha Wilaya ya Songwe tarehe 05 Februari, 2017



Msanii wa Kikindi ... akisoma risala kwa Mkurugenzi wa Wilaya.

 Msanii .. alisema lengo la kuandaa filamu hiyo ni  kudumisha umoja na mshikamano kati ya wasanii na jamii, kutafuta soko la pamoja la sanaa, kulinda na kuendeleza utamaduni  na pia kushirikiana na taasisi mbalimbali zitakazokuwa tayari kusaidia uboreshaji wa sanaa kwa lengo la kujiongezea thamani na kuunganishwa na masoko yenye uhakika



Elias Nawera akipokea nakala ya risala baada ya kusomewa

 Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya akiongea na Wasanii baada ya uzinduzi



Mkurugenzi wa Wilaya akiwa katika picha ya pamoja na Wasanii wa Fighter Artist Group

Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa filamu inayoitwa "Tamati ya dunia

Katika hotuba hiyo Elias Nawera aliwahamasisha  wasanii kuhakikisha kuwa wanasajiliwa ili kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu za nchi, pia wawe na madhumuni mema ya kutumia sanaa kuelimisha jamii na  kujipatia kipato.

 Mwisho aliwasihi wasanii kuwa na kazi nyingine za uzalishaji mali mbali na sanaa kwa kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali ili kunufaika na mkopo  unaotolewa na halmashauri ya wilaya ya songwe kwa lengo kuwawezesha  vijana kujiongezea kipato.


Wednesday, 1 February 2017

ZIARA YA MKUU WA MKOA WA SONGWE KATIKA WILAYA YA MOMBA MKOANI SONGWE


 Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa akikagua shamba la mahindi katika kijiji cha Mpui, Momba


Mkuu wa Mkoa  alipata muda wa kukagua hali halisi ya mazao mashambani  ambapo alitembelea shamba la J. Nziku na kuona jinsi mazao yalivyostawi kuonesha hali nzuri ya mvua katika maeneo hayo.

Akizungumza kuhusu hali ya chakula  Chiku Gallawa alisema,  Mkoa umejipanga vizuri na uemewaagiza Maafisa Biashara kutoka maofisini na kuhakikisha wanatafuta masoko ya mazao ya uhakika, na   Maafisa ugani ambao ni Wataalam wa Kilimo na Maendeleo ya Jamii kuwaelimisha Wakulima mbinu za kilimo bora, kuongeza thamani mazao na kuwashauri watumiea mavuno yao kwa matumizi sahihi na siyo kutumia mazao yao kwa kupikia Pombe ambayo kwa uhalisia haina faida zaidi ya kuleta ugomvi ndani ya familia ambao unamnyima mwanamke haki yake.

 

Mkuu wa Mkoa akiongea na Wananchi wa Kijiji cha Mpui wilayani Momba

Mkuu wa Mkoa akimkabidhi mwanafunzi wa Shule ya Msingi ya Mpui fedha ya kununulia viatu vya shule




Mratibu wa Mradi wa Mkoa wa Songwe Kabambagusha E. akiongea na wanufaika wa fedha za Mfuko wa Jamii (TASAF) katika kijiji cha Mengo , Ndalambo, Momba.


Wanufaika wa TASAF katika kijiji cha Mpui Momba


Mnufaika wa TASAF Bibi Kasambala akitoa ushuhuda wake jinsi alivyonufaika na fedha za Mfuko wa TASAF.  " Mimi nimenunua Kuku, na fedha zingine nimeongezea kununulia bati, sasa nakaa kwenye nyumba iliyoezekwa kwa bati" alieleza Bibi huyo anayeishi katika kijiji cha Kakozi, Ndalmbo, Momba.


Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Momba Adrian Jungu akiongea na wanufaika  wa TASAF katika kijiji cha Luasho, Momba

Mtaalam kutoka Sekretarieti ya Mkoa Mwankenja akiongea na Wanufaika wa Fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  katika Kijiji cha Luasho, Momba

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa  atembelea wanufaika wa fedha za TASAF katika wilaya ya Momba.

Na Mwandishi wetu.


 Mkuu wa mkoa wa Songwe Chiku Gallawa akiwa katika ratiba yake ya  kufuatilia shughuli za maendeleo ya Wananchi katika ngazi ya vijiji, alitembelea Kijiji cha Mpui ampapo alipata fursa ya kuongea na Wanufaika  wa Mfuko wa  Maendeleo ya Jamii (TASAF)  na kujua namna wanavyonufaika na fedha hizo ikiwa ni pamoja na changamoto zake.


Baada ya kuwasikia wanufaika hao, ambao wengi wao walitumia fedha hizo kwa ajili ya kununulia chakula, kusomeshea watoto, kununua Kuku kwa ajili ya kufuga na wachache kununulia bati kwa ajili ya kuezekea nyumba, Mkuu wa mkoa alikuwa na haya ya kusema.

“ Fedha zinazotelewa na Mfuko wa  wa TASAF zifanye malengo yaliyokusudiwa” alisema haya baada ya kusikia kuwa kuna wanafunzi 20 ambao wapo katika orodha ya wanufaika lakini hawapati huduma stahili kwa sababu walezi wao wanatumia fedha hizo kwa shughuli zingine,
 Mkuu wa mkoa aliagiza kuwa viongozi wa Serikali ya Kijiji wafuatilie hilo na kuhakikisha kuwa haki inatendeka kwa watoto ili waendelee na masomo na kupata mahitaji yanayostahili.

Vilevile aliwaagiza Viongozi wa vijjiji kuwafuatilia wazazi wanaohamia mashamba ya mbali na kuwapa wanafunzi ugumu wa kuhudhuria masomo wawarejeshe watoto katika maeneo ambayo watahudhuria masomo shuleni kwa urahisi.

Aidha, Chiku Gallawa aliwataka Wataalam na viongozi wa Vijiji kuona umuhimu wa kuwashirikisha wanufaika wa TASAF katika mpango wa ruzuku ya pembejeo  kwa sababu wana sifa za kupata ruzuku na itawasaidia kupata uhakika wa chakula.

Ili kufanya ufugaji wa Kuku wenye tija Mkuu wa Mkoa alikemea ufugaji holela wa kuachia kuku watafute chakula wenye, alisisita ufugaji unaofuata taratibu za ushauri wa Wataalam na kuzingatia chanjo za mifugo kwa wakati.

Mkuu wa Mkoa aliendela kutoa agizo kuwa ni maarufuku kukata miti ovyo na kuchoma mkaa kwa sababu hali ya ukataji miti imeharibu mazingira katika maeneo makubwa ya Mkoa na kama tabia hiyo itaendelea Mkoa utatumbukia katika ukame kwa kukosa mvua za kutosha.  aliongeza kuwa hata kama mtu amepanda mti wake mwenyewe atatakiwa apate kibali kupitia taratibu sahihi za serikali.